
NGUVU ZA MUNGU DAY 02 | Mwl Benjamin Abel
Karibu kwenye siku ya kwanza (Day 01) ya mfungo wa siku 21, chini ya theme kuu: KABOD – The Return of Glory. Leo tunaanza kwa kuweka msingi muhimu: NGUVU ZA MUNGU. Watu wengi wamezoea huduma bila nguvu, ibada bila athari, na maneno bila matokeo. Lakini katika mfungo huu, tunamtafuta Mungu ambaye si wa hadithi bali wa nguvu na ufunuo. 📖 1 Wakorintho 4:20 — “Kwa maana Ufalme wa Mungu hauwi katika maneno, bali katika nguvu.” Katika somo hili utajifunza: ✅ Nguvu za Mungu zinamaanisha nini katika maisha ya muumini ✅ Kwa nini utukufu hauwezi kurudi bila nguvu halisi za kiroho ✅ Jinsi ya kuombea na kuhitaji nguvu za Mungu kwa ufunuo ✅ Hatari ya kuwa na sura ya utauwa bila nguvu Tunaingia kwa maombi, toba, na shauku ya kuona nguvu za Mungu zikirejea katika maisha yetu. Huu ni mwanzo wa mabadiliko ya kweli.
Tunaingia kwa maombi, toba, na shauku ya kuona nguvu za Mungu zikirejea katika maisha yetu. Huu ni mwanzo wa mabadiliko ya kweli.

BENJAMIN ABELmwalimu
Mwl.BENJAMIN ABEL ni mtumishi wa Mungu mwenye neema ya kufundisha kwa ufunuo na kuwafungua watu katika siri za kiroho. Huduma yake inalenga kuwasaidia waumini kugundua hazina za Mungu zilizofichwa kwa ajili ya wakati huu.

Kesha na Kristo is a global night prayer network, inspired by Matthew 26:40. We are committed to awakening hearts through prayer, the Word, and the Gospel of Christ.
- Telephone : +255 765853859
- Email : info@keshanakristo.com
- Address: Kijitonyama, Dar es salaam Tanzania
Quick Message
Recent Blog
- June 26, 2025